Ayah :
41
يُعۡرَفُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ بِسِيمَٰهُمۡ فَيُؤۡخَذُ بِٱلنَّوَٰصِي وَٱلۡأَقۡدَامِ
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
Ayah :
42
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
43
هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
Ayah :
44
يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
Ayah :
45
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
46
وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
Ayah :
47
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
48
ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
Ayah :
49
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
50
فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
Ayah :
51
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
52
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
Ayah :
53
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
54
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
Ayah :
55
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
56
فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
Ayah :
57
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
58
كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
Ayah :
59
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
Ayah :
60
هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
Ayah :
61
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
62
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
Ayah :
63
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
64
مُدۡهَآمَّتَانِ
Za kijani kibivu.
Ayah :
65
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Ayah :
66
فِيهِمَا عَيۡنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Na chemchem mbili zinazo furika.
Ayah :
67
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?