Ayah :
1
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka!
Ayah :
2
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
Ayah :
3
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Ayah :
4
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Ayah :
5
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja!
Ayah :
6
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia?
Ayah :
7
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
Ayah :
8
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi .
Ayah :
9
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa!
Ayah :
10
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza?
Ayah :
11
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Ayah :
12
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke.
Ayah :
13
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Ayah :
14
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Ayah :
15
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Ayah :
16
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema.
Ayah :
17
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Ayah :
18
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
Ayah :
19
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Ayah :
20
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
Ayah :
21
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Ayah :
22
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
Ayah :
23
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Ayah :
24
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Ayah :
25
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Ayah :
26
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Ayah :
27
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Ayah :
28
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani,
Ayah :
29
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende,
Ayah :
30
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Ayah :
31
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama;
Ayah :
32
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Ayah :
33
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele,
Ayah :
34
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
Ayah :
35
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye,
Ayah :
36
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe.
Ayah :
37
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha
Ayah :
38
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
Ayah :
39
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka;
Ayah :
40
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
Ayah :
41
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika,
Ayah :
42
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu