Header Include

Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/id/swahili_barawani

إِنَّآ أَعۡطَيۡنَٰكَ ٱلۡكَوۡثَرَ

Hakika tumekupa kheri nyingi.

Sisi hakika tumekupa kheri nyingi za daima katika dunia na Akhera.
Hakika tumekupa kheri nyingi.

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَٱنۡحَرۡ

Basi swali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi.

Ilivyo kuwa umepewa hayo, basi dumisha Swala kwa Mola wako Mlezi kwa usafi kabisa, na uchinje dhabihu wako kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa aliyo kupa ya ukarimu, na akakukhusisha wewe khasa kwa kukupa kheri.
Basi swali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi.

إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ ٱلۡأَبۡتَرُ

Hakika anaye kuchukia ndiye aliye mpungufu.

Hakika huyo anaye kuchukia ndiye aliye katika na kila kheri.
Hakika anaye kuchukia ndiye aliye mpungufu.
Footer Include