Header Include

Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/id/swahili_barawani

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.

Imeteketea mikono ya Abu Lahab iliyo kuwa ikiwaudhi Waislamu, na yeye mwenyewe amehiliki pia.
Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.

Hayatolindwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu mali yake aliyo kuwa nayo, wala cheo chake alicho kichuma.
Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia Moto wenye mwako.

Ataingia katika Moto unao waka, aungue.
Atauingia Moto wenye mwako.

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

Na mkewe, mchukuzi wa kuni,

Na ataingia pia kwenye Moto mkewe huyo aliye kuwa akibeba masengenyo baina ya watu, kama alivyo ingia yeye (mumewe).
Na mkewe, mchukuzi wa kuni,

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.

Juu ya shingo yake itakuwa kamba ya mtende ya kumtesa.
Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.
Footer Include