Header Include

Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/id/swahili_barawani

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba!

Ewe Muhammad! Soma unayo funuliwa kwa kufunguliwa kwa Jina la Mola wako Mlezi ambaye ni Yeye tu peke yake ndiye Mwenye uweza wa kuumba.
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba!

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu!

Amemuumba mtu kwa ukamilifu wa mwili wake na ilimu kutokana na kipande cha damu ambacho hakina chochote cha kupelekea kujiona bora.
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu!

ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

Endelea na kusoma, na Mola wako Mlezi aliye Karimu kushinda wote, atakutukuza wala hatakudharau.
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

Yeye ndiye ambaye aliye mfunza mtu kuandika kwa kalamu, na wala kwanza hakuwa anajua hayo.
Ambaye amefundisha kwa kalamu.

عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

Amemfunza mtu yasiyo kuwa yanampitia katika mawazo yake.
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri.

Ni hakika kweli mtu hupindukia mpaka na hupanda kiburi mbele ya Mola wake Mlezi
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri.

أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ

Akijiona katajirika.

Anapo jiona si mhitaji, katajirika.
Akijiona katajirika.

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

Ewe Muhammad! Hakika ni kwa Mola wako Mlezi peke yake ndiyo yako marejeo ya wote kwa kufufuliwa na kulipwa.
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ

Umemwona yule anaye mkataza.

Je! Umemwona huyu jeuri
Umemwona yule anaye mkataza.

عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ

Mja anapo sali?

Anaye mzuia mja asisali anapo taka kusali?
Mja anapo sali?

أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

Hebu niambie khabari za jeuri huyu kama yeye yumo katika uwongofu katika huku kuzuia kwake,
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ

Au anaamrisha uchamngu?

Au kwamba ndio anaamrisha uchamngu katika hayo anayo amrisha!
Au anaamrisha uchamngu?

أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ

Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

Niambie khabari za huyu mwenye kukataza anapo yakadhibisha aliyo kuja nayo Mtume, na akapuuza Imani na vitendo vyema!
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

Hivyo hajui kwamba Mwenyezi Mungu anazijua vyema hali zake, naye atamlipa kwazo?
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ

Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

Kwa kumkemea huyu mwenye kuzuia, anaambiwa kama hakuacha hayo anayo yafanya, basi hapana shaka tutamkokota kwa nguvu tukimshika kwa shungi lake la nywele mpaka Motoni!
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ

Shungi la uwongo, lenye makosa!

Hilo shungi lilio juu ya uso wake mwenye kuropokwa uwongo na mwenye athari za ukosefu!
Shungi la uwongo, lenye makosa!

فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ

Basi na awaite wenzake!

Basi yeye awaite wenziwe na watu wa baraza lake wawe ndio wasaidizi duniani au Akhera.
Basi na awaite wenzake!

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Nasi tutawaita Mazabania!

Sisi tutawaita askari wetu wamsaidie Muhammad na walio pamoja naye, na wapambane na huyo mwenye kukanya na wasaidizi wawasukume kwenye Jahannamu!
Nasi tutawaita Mazabania!

كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩

Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!

Kumnyamazisha huyu mwenye kuzuia, wewe usimkubalie kwa hayo anayo kukataza nayo, na dumu juu ya Swala zako, na endelea na sijida zako, na jijongeze kwa Mola wako Mlezi kwa hivyo.
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
Footer Include