TRADUZIONE SWAHILI - Pioneer Translation Center
Traduzione dei significati del Nobile Corano
Tradotta dal team del Pioneer Translation Center in collaborazione con Al-Rabwa Dawah Association e Association for Multilingual Islamic Content Services
وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Ninaapa kwa farasi waendao mbio wakipumua.
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini.
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wakishambulia wakati wa asubuhi.
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Huku wakitimua vumbi.
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Na wakijitoma kati ya kundi.
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika mwanadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapofufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliyomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na habari zao wote!
share_via