TRADUZIONE SWAHILI - Pioneer Translation Center
Traduzione dei significati del Nobile Corano
Tradotta dal team del Pioneer Translation Center in collaborazione con Al-Rabwa Dawah Association e Association for Multilingual Islamic Content Services
وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Ninaapa kwa jua na mwangaza wake!
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuatia!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapolidhihirisha!
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapolifunika!
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliyeijenga!
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliyeitandaza!
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliyeitengeneza!
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake.
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliyeitakasa.
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amehasiri aliyeiviza.
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotovu wao.
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Aliposimama mwovu wao mkubwa.
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipowaambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
share_via