Header Include

斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

QR Code https://quran.islamcontent.com/zh/swahili_barawani

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
Ole wake kila safihi, msengenyaji!

ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ

Ambao unapanda nyoyoni.

Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
Ambao unapanda nyoyoni.

إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ

Hakika huo utafungiwa nao

Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
Hakika huo utafungiwa nao

فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.

Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Footer Include