Header Include

斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

QR Code https://quran.islamcontent.com/zh/swahili_barawani

وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ

Ole wao hao wapunjao!

Wataangamia wanao punja,
Ole wao hao wapunjao!

ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

Ambao wakijipimia wenyewe kwa watu hujitwalia ya kutosha na kuzidi,
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

Na wakiwapimia watu kwa vipimo au mizani huwapunguzia haki yao wanayo stahiki, kwa dhulma!
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

أَلَا يَظُنُّ أُوْلَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa .

Hivyo haiwapitikii katika akili zao hawa wanao punja wenzao kwamba watakuja fufuliwa,
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa .

لِيَوۡمٍ عَظِيمٖ

Katika Siku iliyo kuu!

Katika siku ya vitisho vikuu?
Katika Siku iliyo kuu!

يَوۡمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Siku watapo simama watu kwa amri ya Mola Mlezi wa walimwengu wote na hukumu yake?
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

Wacheni kupunja, na kughafilika na kufufuliwa! Kwani hakika waliyo andikiwa wakosefu katika a'mali zao mbovu, bila ya shaka yamo katika Sijjin.
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ

Unajua nini Sijjin?

Na nini kitakujuvya nini hiyo Sijjin?
Unajua nini Sijjin?

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Kitabu kilicho andikwa.

Hicho ni Kitabu kilicho pigwa mistari baina ya maandishi yake.
Kitabu kilicho andikwa.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

Wataangamia wanao kadhibisha siku itapo kuwa kufufuliwa na kuhisabiwa.
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

Ambao wanaikanusha Siku ya Malipo.
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

Na wala haikanushi Siku ya Malipo ila kila mwenye kupindukia mipaka mwingi wa madhambi.
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

Na akisomewa Aya za Mwenyezi Mungu zenye kutaja kuwepo malipo husema: Huo ni uwongo wa walio tangulia!
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

كَلَّاۖ بَلۡۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

Ewe uliye kiuka mipaka! Wacha kauli hiyo potovu. Bali nyoyo za wenye kupindukia mipaka imegubikwa na ukafiri na maasi waliyo yatenda.
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

كَلَّآ إِنَّهُمۡ عَن رَّبِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّمَحۡجُوبُونَ

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

Hakika ni kweli kuwa hao wanao kadhibisha watazuiliwa siku hiyo rehema ya Mwenyezi Mungu kwa sababu ya maasi waliyo yachuma.
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

ثُمَّ إِنَّهُمۡ لَصَالُواْ ٱلۡجَحِيمِ

Kisha wataingia Motoni!

Kisha hakika hao bila ya shaka wataingia Motoni.
Kisha wataingia Motoni!

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

Kisha wataambiwa kwa kuwakebehi: Hii basi ndiyo adhabu inayo kuteremkieni ambayo mlikuwa mkiikanusha duniani!
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

Ni hakika kuwa vitendo vya watu wema bila ya shaka vimeandikwa katika I'liyyin.
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

Na nini cha kukujuvya nini I'liyyin?
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ

Kitabu kilicho andikwa.

Hicho ni Kitabu kilicho andikwa wazi maandishi yake,
Kitabu kilicho andikwa.

يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Wanakishuhudia walio karibishwa.

Wanakihudhurisha na kukihifadhi Malaika walio kurubishwa.
Wanakishuhudia walio karibishwa.

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema za Peponi,
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Juu ya viti vya enzi, wakiziangalia neema na ukarimu alio wakirimu Mwenyezi Mungu.
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

Utaona katika nyuso zao uchangamfu na mng'aro wa neema.
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

Wakinyweshwa kinywaji safi kilicho hifadhiwa;
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

Kuhifadhiwa huko hakukuzidisha ila uzuri wake. Na kupata neema hizo, basi, na washindanie wanao shindana.
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسۡنِيمٍ

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

Cha kuchanganyia kinywaji hicho ni maji ya Tasniim ya Peponi,
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

Nayo ni chemchem wanao inywa walio kurubishwa si wengineo, katika watu wa Peponi.
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ كَانُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يَضۡحَكُونَ

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

Wale walio kuwa wakibeba madhambi kuipingia Dini walikuwa wakiwacheka kuwakejeli Waumini duniani.
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمۡ يَتَغَامَزُونَ

 Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

Na wakipita Waumini mbele yao basi wao hukonyezana kwa kuwabeza.
 Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓاْ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمُ ٱنقَلَبُواْ فَكِهِينَ

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

Na hao wakosefu wakirejea kwa ahali zao hurejea kwa furaha na kuona ladha kwa vile kuwakejeli Waumini.
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

وَإِذَا رَأَوۡهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

Na wakiwaona Waumini husema: Ama hakika hawa wamepotea kweli kwa kumuamini Muhammad.
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

وَمَآ أُرۡسِلُواْ عَلَيۡهِمۡ حَٰفِظِينَ

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

Wala hao wakosefu hawakutumwa wawe wa kuwahukumu Waumini kwa kuwaongoza au kuwapoteza, wala kuwa ni walinzi wa vitendo vyao.
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

فَٱلۡيَوۡمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنَ ٱلۡكُفَّارِ يَضۡحَكُونَ

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

Basi Siku ya Malipo walio amini watakuwa ndio wa kuwacheka hao makafiri kwa kuwalipizia kile kicheko chao na kejeli yao ya duniani.
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Ilhali wako juu ya vitanda na matakia watakuwa Waumini wakiziangalia neema za Mwenyezi Mungu alizo wapa.
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

هَلۡ ثُوِّبَ ٱلۡكُفَّارُ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?

Je! Makafiri watalipwa huko Akhera kwa waliyo yatenda duniani?
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Footer Include