Header Include

斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

QR Code https://quran.islamcontent.com/zh/swahili_barawani

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

Alikunja kipaji na akageuka!

Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,
Alikunja kipaji na akageuka!

أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ

Kwa sababu alimjia kipofu!

Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.
Kwa sababu alimjia kipofu!

وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ

Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

Au atawaidhika na mawaidha yamfae.
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ

Ama ajionaye hana haja!

Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake,
Ama ajionaye hana haja!

فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ

Wewe ndio unamshughulikia?

Wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.
Wewe ndio unamshughulikia?

وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ

Na si juu yako kama hakutakasika.

Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?
Na si juu yako kama hakutakasika.

وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ

Ama anaye kujia kwa juhudi .

Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu,
Ama anaye kujia kwa juhudi .

وَهُوَ يَخۡشَىٰ

Naye anaogopa!

Naye anamkhofu Mwenyezi Mungu .
Naye anaogopa!

فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ

Ndio wewe unampuuza?

Wewe unampuuza.
Ndio wewe unampuuza?

كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ

Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

Hakika Aya hizi ni mawaidha.
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anaye penda akumbuke.

Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.
Basi anaye penda akumbuke.

فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ

Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ

Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

كِرَامِۭ بَرَرَةٖ

Watukufu, wema.

Walio bora, wema.
Watukufu, wema.

قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ

Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ

Kwa kitu gani amemuumba?

Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?
Kwa kitu gani amemuumba?

مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

Kisha akamsahilishia njia.

Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.
Kisha akamsahilishia njia.

ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ

Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

Kisha apendapo atamfufua.

Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.
Kisha apendapo atamfufua.

كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ

La! Hajamaliza aliyo muamuru.

Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.
La! Hajamaliza aliyo muamuru.

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

Hebu mtu na atazame chakula chake.

Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!
Hebu mtu na atazame chakula chake.

أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا

Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا

Kisha tukaotesha humo nafaka,

Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.
Kisha tukaotesha humo nafaka,

وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا

Na zabibu, na mimea ya majani,

Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.
Na zabibu, na mimea ya majani,

وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا

Na mizaituni, na mitende,

Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,
Na mizaituni, na mitende,

وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا

Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا

Na matunda, na malisho ya wanyama;

Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).
Na matunda, na malisho ya wanyama;

مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ

Basi utakapo kuja ukelele,

Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,
Basi utakapo kuja ukelele,

يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake,
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ

Na mamaye na babaye,

Na mama yake, na baba yake,
Na mamaye na babaye,

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ

Na mkewe na wanawe.

Na mkewe, na wanawe!
Na mkewe na wanawe.

لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha

Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ

Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza,
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ

Zitacheka, zitachangamka;

Zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.
Zitacheka, zitachangamka;

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ

Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ

Giza totoro litazifunika,

Zimegubikwa na kiza na weusi.
Giza totoro litazifunika,

أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ

Hao ndio makafiri watenda maovu

Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.
Hao ndio makafiri watenda maovu
Footer Include