Header Include

斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

QR Code https://quran.islamcontent.com/zh/swahili_barawani

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu!

Ninaapa kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuving'oa vitu kutokana na pahala pao kwa nguvu,
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu!

وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا

Na kwa wanao toa kwa upole!

Na kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuvitoa vitu kwa utaratibu na ulaini,
Na kwa wanao toa kwa upole!

وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا

Na wanao ogelea!

Na kwa kila kilicho pewa mbio za kutekeleza kazi yake kwa sahala na wepesi.
Na wanao ogelea!

فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا

Wakishindana mbio!

Na kwa vinavyo shindania kutimiza waajibu ulio twikwa juu yao kushindania kwa juhudi,
Wakishindana mbio!

فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا

Wakidabiri mambo.

Na vinavyo dabiri, kupanga, mambo na kuyaendesha kwa mujibu wa vilivyo khusishwa,
Wakidabiri mambo.

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka!

Bila ya shaka Saa ya Kiyama itafika; hiyo siku ambayo mpulizo wa mwanzo wa barugumu utavitikisa viumbe vyote,
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka!

تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

Kifuate cha kufuatia.

Na mpulizo huo utafuatiwa na wa pili ambao ndio utakao kuwa wa kufufuliwa watu.
Kifuate cha kufuatia.

قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga!

Siku hiyo nyoyo zitapapatika kwa khofu.
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga!

أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ

Macho yatainama chini!

Macho ya watu yatakuwa na huzuni, manyonge.
Macho yatainama chini!

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

Watu hawa husema duniani kwa kukanya kufufuliwa: Ati tutarudishwa sisi baada ya kwisha kufa, tuumbwe tena kama tulivyo kuwa?
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

Tukisha kuwa mafupa yaliyo chakaa, ati tutarejeshwa tufufuliwe upya?
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

Wanasema, kwa kukanya na kejeli: Kurejea huko kama kukitokea basi ni marejeo ya khasara, na sisi si watu wa kukhasiri.
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

Msidhani kurejea huko ni kuzito. Kwani hayo ni ukelele mmoja tu,
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

Mara maiti wote watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko!
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

Ewe Muhammad! Imekufikilia hadithi ya Musa,
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

Alipo mwita Mola wake Mlezi katika bonde lilio takaswa, linalo itwa "T'uwa"?
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri

Akaambiwa: Nenda kwa Firauni aliye pindukia mpaka katika udhalimu.
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri

فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

Umwambie: Je! Huelekei kut'ahirika?
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

Na mimi nikuongoze upate kumjua Mola wako Mlezi, umwogope.
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

Musa akamwonyesha Firauni miujiza mikubwa.
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi.

Lakini Firauni alimkadhibisha Musa kwa aliyo kuja nayo, na akamuasi kwa aliyo mwitia.
Lakini aliikadhibisha na akaasi.

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

Kisha akamgeuzia mgongo, akenda kujitahidi kumpinga.
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akanadi.

Akawakusanya wachawi, na akawaita watu,
Akakusanya watu akanadi.

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa.
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

Mwenyezi Mungu akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa a.s.
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

Hakika katika hadithi hiyo yapo mawaidha kwa mwenye kumkhofu Mwenyezi Mungu.
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

Enyi mnao kanya kufufuliwa! Kukuumbeni nyinyi ni taabu zaidi au kuziumba mbingu, kuzikusanya sehemu zake zilio tawanyika mbali mbali,
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

Na kunyanyua kimo chake, na zikakaa sawa hazina tafauti wala ila?
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake

Na akatia kiza katika usiku wake, na akautokeza mchana wake ukawa na mwangaza?
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

Na ardhi baada ya hayo akaikunjua, na akaisawazisha, ikasilihi kukaliwa na watu wake?
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

Akatoa ndani yake maji yake yanayo tibuka katika chemchem zake, na ikamiminika mito yake, na ikawa na mimea yake ya chakula kwa ajili ya watu na wanyama;
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا

Na milima akaisimamisha,

Na milima akaithibitisha imara
Na milima akaisimamisha,

مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

Kwa ajili ya manufaa yenu na wanyama wenu mnao wafuga!
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

Kitakapo fika Kiyama ambacho vitisho vyake vitaenea kote,
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

Siku atakapo kumbuka mtu vitendo vyake vya kheri au shari,
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

Na Jahannamu ikadhihirishwa wazi, akaiona kila mwenye macho kuwa ndio malipo,
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

Basi ama mwenye kupita mpaka kwa maasi yake,
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akakhiari maisha ya dunia,

Na akajichagulia nafsi yake maisha yanayo pita njia,
Na akakhiari maisha ya dunia,

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

Basi Moto wa Jahannamu unao babua upepo wake ndio makaazi yake wala hana mengineyo.
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

Na ama mwenye kukhofu ukubwa na utukufu wa Mola wake Mlezi, na akaizuia nafsi yake na matamanio ya kumpumbaza,
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

Basi huyo nyumba ya neema ya Peponi ndio makaazi yake, wala hana penginepo.
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

Ewe Muhammad! Wanakuuliza, ati, khabari za Saa ya Kiyama, itakuwa lini?
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ

Una nini wewe hata uitaje?

Ujuzi wa hayo hauko kwako hata uwatajie.
Una nini wewe hata uitaje?

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

Ujuzi wa hayo uko kwa Mola wako Mlezi tu, si kwa mwenginewe. (Nabii Isa a.s. ambaye Wakristo wanasema ni Mwana wa Mungu, au ndiye Mungu, pia anasimuliwa katika Biblia kuwa hakuijua Saa na Siku ya Kiyama. Injili ya Mathayo inanukulu maneno ya Yesu: "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.")
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

Kwani waajibu wako ni kuwaonya wanao khofu si kuwatangazia wakati wake.
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.

Na wao siku watakayo iona hiyo Saa ya Kiyama ni kama kwamba hawakuishi duniani zaidi kuliko jioni moja tu, au mchana wake.
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Footer Include