Terjemahan Berbahasa Sawahili - Pusat Terjemah Ruwwād
Terjemahan Makna Al-Qur'an al-Karim
Diterjemahkan oleh Tim Pusat Terjemah Ruwwād bekerjasama dengan Kantor Dakwah di Rabwah dan Lembaga Layanan Konten Islami Multibahasa.
ٱلۡقَارِعَةُ
Inayogonga!
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Ni nini inayogonga?
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na ni nini kitachokujulisha ni nini inayogonga?
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo waliotawanywa;
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufu zilizochambuliwa!
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito.
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani zake zitakuwa hafifu.
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na ni nini kitachokujulisha ni nini hiyo?
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!
share_via